Tuesday, January 10, 2012

Athari za kuoa au kuolewa na mtu wa dini nyingine

MAPENZI kati ya watu wenye dini tofauti huweza kuwa makali kuliko hata ya wale wa dini moja. Lakini hakuna kitu kibaya na kichungu kama kukosa upendo na maelewano baada ya kuona na kuishi kama watu wa dini mbili tofuati.

Shetani wa kila aina na majaribu ya kila sampuli huvamia nyumba yenu na mkawa ni watu wanaoishi bila upendo, maelewano wala masikilizano.

Busara na hekima za watu wa kale bado ni muhimu, kwa kuwa yaliyo mengi wamekwishayaona. Usidanganye na lewalewa la pendo la hivi sasa, lakini ukaja kuishi kwenye maisha ya masikitiko na kujuta kwa miaka yote inayobakia katika maisha yako. Kuamua ni kuchagua. Na uamuzi ni wako.

No comments:

Post a Comment