Tuesday, January 10, 2012

Mapenzi na amani katika ndoa baada ya kuwa na watoto

YAPO mambo mbalimbali ya kuzingatia baada ya wanandoa kupata watoto na baadhi yao wakawa wanasoma au wanahitaji malezi nyumbani.

Kwanza, ni muhimu kuwa na mipango na ratiba za shughuli zote za nyumbani kwa upande wa mama na wasaidizi wake. Nyumba yenye upendo na amani aghalabu mambo yake huenda kwa kiasi na wakati maalum na hayaendi kwa kubahatisha.

Mathalani, kwa watoto wanaokwenda shule, nguo zao budi kufuliwa na kupigwa pasi zikawa tayari leo, kama shule ni kesho. Aidha, mahitaji mbalimbali ya wanaokwenda shule huwa yameainishwa na kuandaliwa kabla ya siku yanayotakiwa.

Watoto kama ni wa shule ya siku (wanakwenda na kurudi kula mchana), lazima wakute chakula kiko tayari na sio kiwe kinaandaliwa baada ya watoto kurudi toka shule.

Aidha, masula ya kununua vitu vya matumizi ya nyumbani, usafi na utunzaji nyumba kwa ujumla ni lazima vifate ratiba au utaratibu ambao hauwaingilii wanafamilia akiwemo baba katika shughuli zake nyingine hapo nyumbani.

Na masuala haya ni ya familia. Sio masual aya sanaa na kuigiza. Hakuna kitu kinachoudhi kama wanafamilia kuwa wasafi na wastaarabu pale tu wageni wanapotarajiwa kuja. Usafi na ustaarabu lazima uwe ni sehemu ya kila siku ya familia ya kiungwana.

1 comment: