YAPO mambo mbalimbali ya kuzingatia baada ya wanandoa kupata watoto na baadhi yao wakawa wanasoma au wanahitaji malezi nyumbani.
Kwanza, ni muhimu kuwa na mipango na ratiba za shughuli zote za nyumbani kwa upande wa mama na wasaidizi wake. Nyumba yenye upendo na amani aghalabu mambo yake huenda kwa kiasi na wakati maalum na hayaendi kwa kubahatisha.
Mathalani, kwa watoto wanaokwenda shule, nguo zao budi kufuliwa na kupigwa pasi zikawa tayari leo, kama shule ni kesho. Aidha, mahitaji mbalimbali ya wanaokwenda shule huwa yameainishwa na kuandaliwa kabla ya siku yanayotakiwa.
Watoto kama ni wa shule ya siku (wanakwenda na kurudi kula mchana), lazima wakute chakula kiko tayari na sio kiwe kinaandaliwa baada ya watoto kurudi toka shule.
Aidha, masula ya kununua vitu vya matumizi ya nyumbani, usafi na utunzaji nyumba kwa ujumla ni lazima vifate ratiba au utaratibu ambao hauwaingilii wanafamilia akiwemo baba katika shughuli zake nyingine hapo nyumbani.
Na masuala haya ni ya familia. Sio masual aya sanaa na kuigiza. Hakuna kitu kinachoudhi kama wanafamilia kuwa wasafi na wastaarabu pale tu wageni wanapotarajiwa kuja. Usafi na ustaarabu lazima uwe ni sehemu ya kila siku ya familia ya kiungwana.
Tuesday, January 10, 2012
Athari za kuoa au kuolewa na mtu wa dini nyingine
MAPENZI kati ya watu wenye dini tofauti huweza kuwa makali kuliko hata ya wale wa dini moja. Lakini hakuna kitu kibaya na kichungu kama kukosa upendo na maelewano baada ya kuona na kuishi kama watu wa dini mbili tofuati.
Shetani wa kila aina na majaribu ya kila sampuli huvamia nyumba yenu na mkawa ni watu wanaoishi bila upendo, maelewano wala masikilizano.
Busara na hekima za watu wa kale bado ni muhimu, kwa kuwa yaliyo mengi wamekwishayaona. Usidanganye na lewalewa la pendo la hivi sasa, lakini ukaja kuishi kwenye maisha ya masikitiko na kujuta kwa miaka yote inayobakia katika maisha yako. Kuamua ni kuchagua. Na uamuzi ni wako.
Shetani wa kila aina na majaribu ya kila sampuli huvamia nyumba yenu na mkawa ni watu wanaoishi bila upendo, maelewano wala masikilizano.
Busara na hekima za watu wa kale bado ni muhimu, kwa kuwa yaliyo mengi wamekwishayaona. Usidanganye na lewalewa la pendo la hivi sasa, lakini ukaja kuishi kwenye maisha ya masikitiko na kujuta kwa miaka yote inayobakia katika maisha yako. Kuamua ni kuchagua. Na uamuzi ni wako.
Subscribe to:
Posts (Atom)