MALEZI ya mtoto huamua kwa kiasi kikubwa mtoto atakuwa na tabia gani. Kwa mfano, mtoto ambaye mama yake hajali yuko wapi saa zote hatoacha kuja kuwa mzururaji. Na mtoto nayeomba hela kutoka kwa watu asiowajua hatoacha na yeye kuja kuwa mtu asiye na aibu kama ombaomba.
Aidha, mtoto anayeruhusiwa kwenda anakotaka, aghalabu, hukutana na mengi yasiyo ya kawaida. Ndivyo inavyotokea kwa watoto wanaokwenda nyumba zenye wabwia unga ana hatari ya kuonjeshwa huo unga. Na kama tunavyojua mtoto akishauonja atataka tena na tena. Kuanzia hapo utakuwa huna mtoto.
Hali kadhalika mtoto wa kike anayeachiwa kujihusisha na changudoa ni vigumu yeye kuwa salama. Atakuwa anayaona hayo anayoyaona na kwa kuwa yeye ni binadamu atataka kujaribu. Akijaribu na akiona utamu basi utakuwa tena umekwishampoteza mtoto. Sidanganyiki bora zaidi ni ile ya kumlea mtoto awe mbali na mambo machafu na ya hatari.
Tuesday, December 1, 2009
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment